Barua ya Ommy dimpoz iliyoleta utata Instagram

Hakuna jambo baya kama unafiki.. Wewe Mubenga na yoyote anaejifanya Ommy amekosea kuingiza Wazazi ni unafiki Mkubwa. Ommy kutukanwa kama Shoga hakumuumizi mzazi wake?! Kumtukana Maumbile yake sio Kumuhusisha Mzazi? Maana mzazi ndiye aliyemzaa Ommy sasa kumtukana mwanae Maumbile yake ambayo amemzaa nayo hamumfanyi Yule Mama akajisikia vibaya? Hivyo sio kumuhusisha? Kwanini tu msiseme Ommy na Mziki wake mnasema Maumbile yake? Unamaanisha nini? Si akutukanae hakuchagulii tusi? Basi Tulieni Mchambuliwe kama karanga.. Huyo Mtu wenu ndio anaemfanya Mama yake akawa ndani ya hili sekeseke... Watu wamemuacha kimya na Kiki zake, anawashwa hawezi kuishi bila Mme wake Ali kaanzisha vurugu.. Jamani bado mnasema kaonewa.. Muache aone utamu wa kukaa na kutaka kudhalilisha watu muda wote.. Amezoea, muache nae aonje raha ya kudhalilishana. Anaweza kujifunza kutoka hapo. Akitafuta hizo Kiki zake atazitafuta kwa adabu.. Tuacheni mnafki, kwenye vita hatuchaguliani silaha.. Kavuka mipaka ya kumtukana mwenzie Maumbile yake, kwanini nae watu wamuangalie..? Mubenga, mamlaka zipi unazoziongelea zinazosapoti mtu kutukanwa shoga na Maumbile yake? Unaongea habari gani ama unataka tu uropoke uonekane na wewe upo kwenye Ramani? Tuliza makalio, acha shobo.. Kama mngekuwa na heshima na nidhamu kwa wazazi wala hata msingeanzisha chokochoko.. Mnaanzisha kosovo za mawe kumbe nyumba za vioo.. Mtafuraia hasara tu, hakuna namna...!! Sasa mwambieni Kaka yenu ajibu tena, yeye si kavurugwa anajua kutafuta Kiki.. mnafikiri kila kitu kiki.. Sasa Kiki ataipata na majasho yatamtoka vilevile.. hakuna kitu cha bure.. Tuondeleeni unafiki sisi.. Hivi kwanza Nani anaongoza kudhalilisha dada zetu/mama zetu kama Domo? Sio yeye aliyekuwa anamdhihaki Wema na kutokuzaa? Sio yeye juzi tu hapa alimuita mwanamke mwenye watoto wawili, dada yetu Hamisa #BITCH - au Hamisa yeye sio mama? Ufupi tu kama Kimba! #VitaNiVitaMuraa
A post shared by King Of BongoFlava (@alikiba_blood_fans) on
Copyright © Jaffa the Done Entertainment and Music Website . Designed by OddThemes & SEO Wordpress Themes 2018